UGONJWA WA HOMA YA INI NA MAMBO MUHIMU YA TUPASAYO KUFAMU.
INI ni nini ??
INI ni kiungo muhimu sana katika miili yetu, hufanya kazi nyingi sana zaidi ya kazi 500; Moja ya kazi kubwa ya Ini katika miili yetu ni Kuchuja na Kuondoa Sumu kutoka kwenye Damu.
kutokana na sababu mbalimbali zinzo sababisha miili yetu kukusanya sumu katika damu kama vile, UNYWAJI WA POMBE KUPITA KIASI, SUMU KWENYE DAMU,Au MAAMBUKIZI; husababisha ini hupata shida na kuvimba: hivyo INI hushindwa kufanya kazi za kila siku katika miili yetu.
hii hali huitwa HOMA YA INI au HEPATITIS.
VIRUSI WA HOMA YA INI NI WEPI??
Katika Bara letu la Afrika, maambukizi ya ya virusi wa homa ya ini ndio sababu kuu ya shida kwenye INI. Virusi vya homa ya Ini vipo vya aina 5 ( A,B,C,D,E.)
Aina mbili za virusi ( B na C) ndio sababu kuu ya ugonjwa wa INI na husambaa kwa njia mbili, ambazo ni Damu na Maji maji ya mwilini, kama vile jasho, shahawa,mate na mengineyo.
virus aina B huambukizwa kwa kupitia damu kutoka kwa mtu mwenye maambukizi ya virusi vya homa ya ini kundi B kwenda kwa mtu ambaye hana maambukizi,. hii yaweza kuwa ni kwa kuchangiwa damu iliyo kuwa haijapimwa kikamilifu vimelea vya homa ya INI, au kuchangia vitu vyenye ncha kali kutoka kwa mtu aliye ambukizwa kwenda kwa mtu asiye na maambukizi.
Virus aina C huambukizwa kwa kupitia mgusano wa majimaji ya mwili kutoka kwa mtu mwenye maambukizi ya ugonjwa wa homa ya INI kwenda kwa mtu asiye na maambukizi ya ugonjwa wa homa ya INI.
DALILI KWA MTU MWENYE UGONJWA WA HOMA YA INI.
Dalili za mu mwenye maambukizi ya ugonjwa wa HOMA YA INI zimegawanyika katika sehemu kuu mbili ambazo ni ( dalili za muda mfupi- ACUTE HEPATITIS) na Dalili za KUDUMU ( CHRONIC HEPATITIS)
Dalili hizi za mwanzo huanza kutokea ndani ya miezi 6 baada ya mtu kuambukizwa virusi vya homa ya INI. Hata hivyo dalili hhizi huweza kutokea kwa baadhi ya watu na sio kwa kila mtu. hivyo uonapo dalili hizi tafadhari fika kituo cha kutolea huduma kilicho karibu nawe.
1.kupoteza hamu ya kula
2. kichefuchefu na kutapika
3. mwili kuuma
4. mkojo kuwa na rangi iliyo kolea kama Coca - Cola
5. kupata manjano kwenye macho, viganja vya mikono/ kucha au mwili mzima.
6. kuvimba tumbo na kupumua kwa shida.
Dalili za kudumu: ( Chronic Hepatitis) - watu wenye maambukizi ya kudumu ya virusi vya homa ya ini, mara nyingi huwa hawana dalili. kadri muda unavyo enda virusi husababisha INI kusinyaa(CIRRHOSIS) na kushindwa kabisa kufanya kazi vyema.
Pia maambukizi ya virusi vya Homa ya INI huchangia kupata SARATANI YA INI.
MAKUNDI YALIYO KATIKA HALI HATARISHI KUPATA MAAMBUKIZI YA HOMA YA INI.
Haya ndio makundi ya watu walio katika nafasi kubwa sana ya mkuweza kupata maambukizi ya virusi vya ugonjwa wa INI.
- watoto wote
- watu wote wanao tumia dawa za kulevya na kujidunga.
- watu wote ndani ya familia wanao ishi na mtu mwenye virusi vya homa ya INI.
- watu wote wanao fanya biashara ya ngono.
- watu wote wanao kunywa pombe kupitiliza.
- watu wenye wapenzi wengi
- watumishi wote wa idara ya afya
- Chanjo ya kwanza pale tu, unapo pima na kukuta hauna maambukizi ya Virusi vya Homa ya Ini.
- sindano ya pili hutolewa baada ya mwezi mmoja tangu ulipo choma chanjo ya kwanza.
- sindano ya tatu baada ya miezi sita tangu ulipo choma chanjo ya kwanza.
Asante kwa elimu hii Daktari, nikitaka chanjo utaratibu upoje?
ReplyDeletechanjo zina patikana vituo vyote vya kutolea huduma za afya TANZANIA
DeleteUmetisha sana Jamaa Keep it content ni Nzuri, zinaeleweka kwa kila mtu
ReplyDelete